sw_tn/isa/55/12.md

1.1 KiB

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

kuongozwa mbele kwa amani

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitakuongoza mbele kwa amani"

milima na vilima itabomoka kwa kelele za shangwe mbele yako, na miti yote ya shambani itapiga makofi

Yahwe anazungumzia milima, vilima na miti kana kwamba vilikuwa watu na sauti na mikono, vikisherehekea pale Yahwe anapowaokoa watu wake.

Badala ya miba ya vichaka, mvinje utaota; na badala ya mtemba, mti wa mihadasi utaota

Maneno "miba ya vichaka" na "mvinje" ina maana ya aina ya mimea ambayo ina miba mikali inayoota juu yao. Maneno "mvinje" na "mtemba" una maana ya aina ya miti ya kijani. Mimea ya miba inaashiria ukiwa, wakati ukijani unaashiria uzima na mafanikio.

kwa jina lake

Hapa neno "jina" linawakilisha umaarufu wa Yahwe. "kwa umaarufu wake" au "kwa heshima yake"

ambayo haitakatwa mbali

Kitu kinachokoma kuwepo kinazungumziwa kana kwamba kinakatwa mbali, kama tawi linavyokatwa mbali na mti au kipande cha kitambaa kinavyokatwa kutoka kwenye nguo. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambalo halitafika mwisho" au "ambalo itadumu milele"