sw_tn/isa/55/02.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Kwa nini unapima uzito wa fedha kwa kile kisicho mkate?

Yahwe anauliza swali hili kukaripia watu. Anazungumza juu ya watu kutafuta furaha kando na Yahwe kana kwamba walikuwa wakinunua vitu kula ambavyo havikuwa chakula. "Haupaswi kupima fedha kwa kile ambacho ni mkate"

unapima uzito wa fedha

Hii ina maana ya kuhesabu sarafu za fedha ili kumlipa mtu kwa ajili ya kitu. "lipa pesa"

kwa kile kisicho mkate

Hapa neno "mkate" unawakilisha chakula kwa ujumla. Inadokezwa ya kwamba watu walikuwa wakinunua vitu kula ambavyo havikuwa chakula halisi. "kwa vitu vya kula ambavyo sio chakula halisi"

kwa nini unafanya kazi kwa kile hakiridhishi?

Yahwe anauliza swali hili kukaripia watu. Anawazungumzia kutafuta furaha tofauti na kwa Yahwe kana kwamba walikuwa wakifanya kazi kupata pesa kununua vitu ambavyo haviwezi kuwaridhisha. "haupaswi kufanya kazi kwa ajili ya pesa kutumia kwa vitu ambavyo haviridhishi"

kula kilicho chema, na ufurahie katika unene

Watu kumtumaini Yahwe kwa kumbariki na furaha inazungumziwa kana kwamba wanakula chakula kizuri ambacho kinawafanya wawe na furaha.

katika unene

Neno "unene" lina maana ya nyama ambayo ina mafuta mengi juu yake na ni lahaja kwa chakula kizuri. "kwa vyakula vizuri"