sw_tn/isa/53/01.md

1.0 KiB

Maelezo ya Jumla

Hapa Isaya anafafanua matukio ambayo yatatokea katika siku za usoni kana kwamba yametokea kipindi cha nyuma. Hii inasisitiza ya kwamba yatatokea hakika.

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua mtumishi wa Yahwe.

Ni nani aliyeamini kile walichosikia kutoka kwetu

Kile ambacho Yahwe amegundua ni ajabu sana hadi anashangaa kama walio uhamishoni wataamini. "walichosikia" inajumlisha yeye na wale walio uhamishoni. "Ni vigumu kw yeyote kuamini kile alichosikia"

na ni kwa nani mkono wa Yahwe umefunuliwa?

Mkono una maana ya nguvu ya Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na Yahwe amefunua nguvu yake kwa watu"

Kwa maana alikua mbele ya Yahwe kama mti mchanga

Hapa "alikua" ina maana ya mtumishi wa Yahwe ambaye Isaya anamlinganisha na mti mchanga sana. Hii inasisitiza ya kwamba ataonekana dhaifu.

kutoka katika nchi iliyokauka

"nchi iliyokauka" ni ardhi ngumu na iliyokauka ambayo hairuhusu mimea kuota na inawakilisha wapi mtumishi wa Yahwe atakuja. "kutoka katika hali isiyowezekanika"