sw_tn/isa/52/05.md

1.5 KiB

Basi sasa nina nini hapa ... kuona ya kwamba watu wangu wanachukuliwa bure?

Yahwe anatumia swali kufanya watu kuzingatia kwa makini kile anachotaka kusema. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriiwa kama kauli. "Basi sasa tazama kile kinachotokea ... watu wangu wanachukuliwa tena bure"

nina nini hapa - hili ni tamko la Yahwe - kuona

Maana zaweza kuwa 1) Yahwe anasema, "hili ni tamko la Yahwe". "Ninalo hapa - hiki ndicho kile nachotamka- kuona" au 2) Isaya anasema, "Hili ni tamko la Yahwe". "Ninalo hapa, anatamka Yahwe, "kuona"

kuona ya kwamba watu wangu wanachukuliwa bure

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Ninaona adui akichukua watu wangu bure"

bure

Maana zaweza kuwa 1) "bure" ina maana Wababeli walichukua watu bila haki na bila sababu au 2) hii inaendelea sitiari kutoka 52:2 ambapo Yahwe anazungumziwa kana kwamba alimiliki watu wa Israeli na anaweza kuwatoa bure.

Wale wanaotawala juu yao wanadhihaki

Hii ina maana ya Wababeli ambao wamewashinda watu. Hata hivyo, baadhi ya tafsiri zina, "Wale ambao hutawala juu yao wanalia". Kwa tafsiri hizi, kipande hiki kina maana ya viongozi wa Waisraeli walio katika kifungo.

jina langu linakashifiwa mfululizo siku nzima

Hapa "jina" inawakilisha sifa ya Yahwe. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "wale ambao hutazama aduii akichukua watu wangu wanaendelea kusema mambo mabaya juu yangu"

Kwa hiyo watu wangu watalijua jina langu

Hapa "jina" inawakilisha sifa ya Yahwe. "Kwa hiyo watu wangu watanijua mimi ni nani kiukweli"