sw_tn/isa/51/17.md

1.5 KiB

Amka, amka, simama, Yerusalemu

Hapa "Yerusalemu" inawakilisha watu wanaoishi pale. Yahwe anazungumzia watu wa Yerusalemu kana kwamba walikuwa wakimsikiliza. "Amka, amka, simama, nyie watu wa Yerusalemu"

Amka, amka, simama

"Uwe tayari na inuka". Kurudia kwa neno "amka" linasisitiza uharaka wa wito kuamsha watu wa Israeli. Hautumiki kuwaamsha kutoka usingizi halisi.

wewe ambaye umekunywa kutoka katika mkono wa Yahwe ... kutoka katika kikombe cha kupepesuka

Yahwe anazungumzia kuwaadhibu watu wake kana kwamba alikuwa amewalazimisha kunywa kutoka katika bakuli ambalo lilijazwa na hasira yake. Na walipokunywa bakuli la hasira yake, walipepesuka kana kwamba walikunywa mvinyo mwingi.

chini mpaka kwenye masimbi

Neno "masimbi" lina maan ya vipande vya chini ya chombo ambacho kinywaji kilkuwemo. "mpaka chini kabisa"

kutoka katika mkono wa Yahwe

Hapa Yahwe anamaanishwa kwa mkono wake kusisitiza ya kwamba yeye ndiye aliyetoa bakuli kwa watu wake. "ambayo alikupatia"

katika kikombe cha kupepesuka

"kutoka katika kikombe ambacho kimesababisha upepesuke kana kwamba ulilewa kwa mvinyo"

kupepesuka

kutotembea wiima, au kujikwaa akiwa anatembea

Hakuna mtu ... wa kumuongoza; hakuna mtu ... kumchukua kwa mkono

Vishazi hivi viwili vina maana moja na vinaweza kujumlishwa. Hii inazungumzia Yerusalemu kutojiweza kana kwamba mji uliikuwa mwanamke mlevi bila mtoto wa kumsaidia kutembea kwa usalama. "Hauna mtu wa kukusaidia! Wewe ni kama mwanamke mzee aliyelewa asiye na mwana kumchukua kwa mkono na kumuongoza"