sw_tn/isa/51/14.md

982 B

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Israeli.

Yule ambaye ameinamishwa chini

Hii ina maana ya watu wa Israeli ambao ni watumwa wa Babeli. Msemo huu unafafanua namna wanvyofanya kazi. "Mtumwa"

shimo

Hii ina maana ya Kuzimu. "shimo la kuzimu" au "kaburi"

wala hatapungukiwa mkate

Hapa "mkate" unawakilisha chakula kwa ujumla. Hii inaweza kuandikwa kwa hali ya chanya. "wala atakuwa bila chakula"

ambaye huvurugavuruga bahari

Hii inazungumzia Yahwe kusababisha bahari kusogea na mawimbi kuinuka na kuanguka kana kwamba alikuwa akikoroga bahari kama mtu anavyokoroga ujazo wa bakuli kwa kijiko kikubwa. "ambaye anasababisha bahari kuvurugwa" au "ambaye hufanya bahari kusogea juu na chini"

mawimbi yake yaungurume

Muungurumo ni sauti ya juu ya nguvu unayofanywa na kitu chenye uhai, kama vile dubu au simba. Hapa mawimbi yanaelezwa kama kutengeneza sauti ya nguvu. "mawimbi huanguka kwa sauti"

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi ya Israeli.