sw_tn/isa/51/04.md

1.4 KiB

Maelezo ya Jumla

Yahwe anazungumza na watu wa Israeli.

Kuwa msikivu kwangu ... nisikilizeni mimi

Misemo hii miwili ina maana moja. Kwa pamoja inaimarisha amri ya kusikiliza.

Nitafanya haki yangu kuwa mwanga kwa ajili ya mataifa

Hapa haki ya Mungu inawakilisha sheria yake, na mwanga unawakilisha maarifa ya kilicho sahihi. Hii ina maana watu wa mataifa wataelewa na kutii sheria ya Mungu. "sheria yangu utafundisha mataifa kilicho sahihi" au "mataifa watajua sheria yangu"

Haki yangu ipo karibu

Wazo la "karibu" inawakilisha "hivi karibuni". Haki ya Mung kuwa karibu inawakilisha yeye kuonyesha haki yake hivi karibuni. Atafanya hivi kwa kutimiza ahadi zake na kukomboa watu. "Hivi punde nitaonyesha haki yangu"

wokovu wangu utatoka nje

Mungu anazungumzia kuwaokoa watu kana kwamba wokovu wake ulikuwa kitu ambacho kinaweza kutoka nje kwao. "Nitaokoka watu"

mkono wangu utahukumu matafa

Hapa mkono wa Mungu unawakilisha nguvu yake, na kuhukumu inawakilisha utawala. "Nitatawala mataifa kwa nguvu yangu"

pwani

Hii ina maana ya watu ambao wanaishi katika pwani ya nchi za mbali kupita bahari. "watu amboo wanashi katika pwani" au "watu ambao wanaishi katiak nchi kupita bahari"

watasubiri kwa shauku kwa ajili ya mkono wangu

Hapa mkono wa Mungu unawakilisha kile atakachofanya. Hapa ina maana ya yeye kokoa watu. "watasubiri kwa shauku kwangu kufanya kitu" au "watanisubiri kwa shauku niwaokoe"