sw_tn/isa/50/05.md

948 B

Taarifa ya Jumla

Mtumishi wa Yahwe anaendelea kuzungumza.

Bwana Yahwe amefungua sikio langu

Yahwe kumwezesha mtumishi wake kusikia na kuelewa inazungumziwa kana kwamba Yahwe alifungua sikio lake. "Bwana Yahwe ameniwezesha kumsikia na kumwelewa"

na sikuwa muasi, wala sikugeuka kinyume

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Kutotii kile ambacho Yahwe alisema inazungumzwa kana kwamba ilikuwa kugeuza mgongo wa mtu kwake. Hii inaweza kuelezwa katika misemo chanya. "na nikatii kile alichosema"

Niliwapa mgongo wale walionipiga, na mashavu yangu kwa wale walionyofoa ndevu zangu

Kuruhusu watu kumpiga na kunyofoa ndevu zake inazungumziwa kana kwamba ilikuuwa kutoa mgongo wake na mashavu kwao. "Niliruhusu watu kunipiga mgongoni na kunyofoa ndevu zangu kutoka mashavuni mwangu"

Sikuficha uso wangu kutoka kwa matendo ya aibu na kutemewa

Kuficha uso wa mtu ina maana ya kujilinda. "Sikujihami pale waliponidhihaki na kunitemea"