sw_tn/isa/50/04.md

897 B

Taarifa ya Jumla

mtumishi wa Yahwe anaanza kuzungumza.

Bwana Yahwe amenipatia ulimi kama wale wanaofundishwa

Neno "ulimi" linawakilisha kile anachosema. Maana zaweza kuwa 1) Yahwe amemwezesha kuzungumza kama mtu ambaye amejifunza kuzungumza kwa ustadi. "Bwana Yahwe ameniwezesha kuwa msemaji mwenye ujuzi" au 2) Yahwe kanifundisha kile nachosema. "Bwana Yahwe ameniwezesha kuzungumza kile alichonifundisha"

anaamsha sikio langu kusikia

Hapa "sikio langu" ina maana ya mtumishi wa Yahwe. Yahwe kumwezesha kusikia na kuelewa kile ambacho Yahwe anafundisha inazungumziwa kana kwamba Yahwe aliamsha sikio lake kutoka usingizini. "ameniwezesha kuelewa kile anachosema"

kama wale wanaofundishwa

Mtumishi anajilinganisha na mwanafunzi ambaye hujifunza kutoka kwa mwalimu wake. Maana zawekana kuwa 1) "kama mtu ambaye hujifunza kutoka kwa mwalimu wake" au 2) "kama mtu ambaye amemfundisha"