sw_tn/isa/50/02.md

1.6 KiB

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzunguza na watu wa Israeli.

Kwa nini nilikuja lakini hapakuwa na mtu kule? Kwa nini niliita lakini hakuna aliyejibu?

Sentensi hizi mbili kimsingi zina maana moja. Yahwe anatumia maswali kusisitiza ya kwamba watu wapo uhamishoni kwa sababu hawakuitikia kwake, sio kwa sababu hakuwa tayari kuwaokoa. "Nilipokuja kwako, ulipaswa kuwa pale, lakini haukuwepo. Nilipokuita, ulitakiwa kujibu, lakini haukujibu". au "Nilipokuja kuzungumza na wewe, haukuniitikia".

Je! mkono wangu ulikuwa mfupi sana kukukomboa? Je! hapakuwa na nguvu ndani mwangu kukuokoa?

Yahwe anatumia maswali mawili ya kufanana kukaripia watu kwa kuamini ya kwamba hakuwa na nguvu ya kutosha kuwaokoa. "Mkono wangu hakika haukuwa mfupi kwangu kukulipia, na nilikuwa na uwezo kukuokoa!" au "Hakika nina uwezo wa kuwaokoa kutoka kwa adui wako"

Je! mkono wangu ulikuwa mfupi sana

Hapa neno "mkono" unawakilisha nguvu ya Yahwe. Yahwe kutokuwa na nguvu ya kutosha inazungumziwa kana kwamba mkono wake ulikuwa mfupi. "Je! sikuwa na nguvu ya kutosha"

Je! hapakuwa na nguvu ndani mwangu

"Je! sikuwa na nguvu"

naifanya mito kuwa jangwa

Yahwe anazungumzia kukausha mito kana kwamba alikuwa akigeuza kuwa jangwa. "Ninafanya mito kukauka kama jangwa"

samaki wao hufa kwa kukosa maji na kuoza

"samaki wao hufa na kuoza kwa kukosa maji". Neno "wao" ina maana ya bahari na mito.

naivisha mbingu kwa giza; naifunika kwa nguo ya gunia

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja. Yahwe inazungumza kusababisha mbingu kuwa na giza kana kwamba alikuwa akiivika kwa nguo ya gunia. "Ninafanya mbingu kuwa giza, kana kwamba ilikuwa ikivaa nguo nyeusi ya gunia"