sw_tn/isa/50/01.md

1.1 KiB

Hati ya talaka ambayo nilimuacha mama yako iko wapi?

Yahwe anazungumza juu ya Sayuni kana kwamba mji ulikuwa mama wa watu walioishi kule na kutuma watu katika uhamisho kana kwamba alikuwa akitoa talaka kwa mama yao.

Hati ya talaka ambayo nilimuacha mama yako iko wapi?

Yahwe anauliza swali hili la balagha ili kwamba watu watoa "hati ya talaka" ambayo ingetoa sababu ya Yahwe kuwatuma katika uhamisho. "Nionyesheni hati ya talaka mabyo nilimuacha mama yenu"

Ni wadai wapi wa kwangu nimekuuza?

Yahwe anazungumzia kuwafukuza watu katika uhamisho kana kwamba alikuwa akiwauza.

Ni wadai wapi wa kwangu nimekuuza?

Yahwe anauliza swali hili kusisitiza ya kwamba hakuwauza kwa sababu alikuwa na deni kwa mdaiwa. Inadokezwa ya kwamba hiki ndicho watu walivyofikiri. "Sikuwauza kwa sababu ninadaiwa na mtu"

uliuzwa kwa sababu ya dhambi zako, na kwa sababu ya uasi wako, mama yako alifukuzwa

Yahwe anatoa sababu ya kuwafukuza watu katika uhamisho, ambayo anazungumzia kana kwamba amewauza na kutengana na mama yao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nilikuuza kwa sababu ya dhambi zako, na nikatengana na mama yako kwa sababu ya uasi wako"