sw_tn/isa/49/26.md

989 B

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na Sayuni kana kwamba ilikuwa mtu.

Nitawalisha wakandamizaji wako kwa nyama yao wenyewe

Maana zaweza kuwaa 1) wakandamizaji watakuwa na njaa sana watakula nyama ya rafiki zao waliokufa. "Nitasababisha wakandamizaji wako kula nyama yao wenyewe" au 2) Yahwe anazungumzia wakandamizaji kupigana dhidi yao wenyewe na kujiangamiza kana kwamba walikuwa wakijila wenyewe. "Nitasababisha wakandamizaji wako kujiangamiza wao wenyewe, kana kwamba walikuwa wakila nyama yao wenyewe"

na watalewa katika damu yao wenyewe, kan kwamba ilikuwa divai

Maana zaweza kuwa 1) wakandamizaji watakuwa na kiu sana mpaka watakunywa damu ya rafiki zao ambao wamekufa. "na watakunywa damu ya rafiki zao na kuwa kama watu dhaifu waliolewa divai" au 2) Yahwe anazungumzia wakandamizaji kupigana dhidi yao wenyewe na kujiangamiza kana kwamba walikuwa wakinywa damu ayo wenyewe. "na watamwaga damu nyingi sana ya rafiki zao kana kwamba walikuwa wakilewa na divai"