sw_tn/isa/47/14.md

669 B

Kauli Unganishi

Yahwe anaendelea kuzungumza na Babeli kuhusu anguko lake kana kwamba alikuwa malkia ambaye ameaibishwa.

watakuwa kama mashina ya mabua. Moto utawaunguza

Yahwe analinganisha waganga na wachawi na mabua ambayo huwaka haraka katika moto. Hii ina maana Yahwe atawaangamiza kwa urahisi kama vile moto unavyochoma mashina ya mabua, na kwa hiyo hawana nguvu ya kuokoa Babeli.

mkono wa mwale wa moto

Hapa neno "mkono" unawakilisha nguvu. "nguvu ya mwale wa moto"

Hakuna mkaa wa kuwapa joto na hakuna moto kwa ajili yao kukaa karibu

Yahwe anasisitiza ya kwamba huu ni moto wa kuharibu kwa kusema kwamba sio moto ambao watu hutumia kujipatia joto.