sw_tn/isa/43/08.md

1.1 KiB

watu ambao ni vipofu ... viziwi

Yahwe anazungumzia wale ambao hawamsikilizi au kumtii kana kwamba walikuwa vipofu na viziwi.

Ni nani kati yao angeweza kutamka hili na kutangaza kwetu matukio ya mapema?

Swali hili la balagha linatumika kwa miungu ambao watu wa mataifa huabudu. Jibu linalodokezwa ni kwamba hakuna kati yao angefanya hivi. Swali hili linaweza kutafsiriwa kama kauli. "Hakuna kati ya miungu yao ingeweza kutamka hili au kutangaza kwetu matukio ya mapema"

kutangaza kwetu matukio ya mapema

Msemo huu una maana ya uwezo wao kusema juu ya matukio ambayo yametokea kipindi cha nyuma kabla hayatokea. "alitangaza kwetu matukio ya mapema kabla hayajatokea"

Waache walete mashahidi wao kujithibitishia wenyewe kuwa sahihi, waache wasikilize na kukiri, "Ni ukweli'.

Yahwe anatoa changamoto kwa miungu ambao mataifa huabudu kutoa mashahidi ambao watashuhudia ya kwamba wameweza kufanya vitu hivi, ingawa anajua ya kwamba hawawezi kufanya hivyo. "Miungu hawa hawana mashahidi ambao watathibitisha kuwa sahihi, mashahidi ambao watasikiliza na kukiri, "Ni kweli"