sw_tn/isa/40/21.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Mungu.

Je! haujajua? Haujasikia? Haijaambiwa kwako toka mwanzo? Haujaelewa toka misingi ya dunia?

Isaya anatumia maswali haya kusisitiza ya kwamba watu wanapaswa kujua ukuu wa Yahwe kma muumba. "Kwa uhakika unajua na umesikia! Imeambiwa kwako toka mwanzo; umeelewa toka misingi ya dunia!"

Haijaambiwa kwako toka mwanzo?

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Je! watu hawajakuambia toka mwanzo?"

toka misingi ya dunia

Nabii anazungumzia Yahwe kuumba dunia kana kwamba dunia ilikuwa jengo ambalo Yahwe alilaza msingi. "kutoka kipindi ambacho Yahwe aliumba dunia"

Yeye ndiye ambaye hukaa juu ya upeo wa macho ya dunia

Nabii anazungumzia Yahwe kutawala dunia kana kwamba Yahwe alikuwa amekaa juu ya kiti cha enzi juu ya dunia.

wakazi ni kama panzi mbele zake

Nabii analinganisha namna ambavyo Yahwe anachukulia wanadamu kwa namna ambavyo wanadamu wangechukulia panzi. Kama vile panzi ni wadogo kwa binadamu, binadamu ni wadogo na dhaifu mbele za Mungu.

Ananyosha mbingu kama pazia na kuitawanya kama hema la kuishi ndani

Mistari hii miwili inatumia maana ya kufanana. Nabii anazungumzia Yahwe kuumba mbingu kana kwamba alisimamisha hema ambalo ataishi. "Anatawanya mbingu kwa urahisi kama mtu anavyonyosha pazia au kusimamisha hema ambalo anishi"