sw_tn/isa/37/28.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kwa mfalme wa Ashuru.

Lakini ninajua kukaa kwako chini, kutoka kwako, kuingia kwako

Hii ina maana ya vitendo vyote vya maisha. "Ninajua kila kitu unachofanya"

na hasira yako dhidi yangu

Neno "hasira" linaweza kuelezwa kama kitenzi. "jinsi unavyokasirika dhidi yangu"

kiburi chako

Hapa "kiburi" cha mfalme kina maana ya maneno yake ya kiburi. "maneno yako ya kiburi"

kiburi chako kimeyafikia masikio yangu

Hii inazungumzia yahwe kusikia maneno ya mfalme kana kwamba maneno ya mfalme yalikuwa kitu ambacho kilisafiri mpaka katika sikio lake. "Nimesikia ukizungumza kwa kiburi"

nitaweka ndoano yangu katika pua yako, na lijamu katika mdomo wako

Mtu hutumia ndoano na lijamu kuongoza mnyama. Hii inazungumzia Yahwe kutawala mfalme kana kwamba mfalme alikuwa mnyama yahwe aliyetawala kwa lijamu na ndoano. "Nitakutawala kama mwanamume anavyotawala mnyama wake kwa ndoano katika pua yake na lijamu katika mdomo wake"

Nitakurudisha katika njia uliyotoka

Hii ina maana ya kusababisha mfalme kurudi katika nchi yake ya nyumbani. Maana ya hii inaweza kuwekwa wazi. "Nitakulazimisha kurudi katika nchi yako mwenyewe"