sw_tn/isa/37/26.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa Yahwe kw mfalme wa Ashuru.

Je! haujasikia jinsi ... nyakati?

Yahwe anatumia swali hili la balagha kumkumbusha Senakeribu kuhusu taarifa ambayo alipaswa kuwa anaifahamu. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Hakika mmesikia jinsi ... nyakati".

Upo hapa kupunguza miji isioingilika katika marundo ya uharibifu

Yahwe alikuwa amepanga kwa jeshi la Senakeribu kuangamiza miji ambayo walikuwa wameangamiza. Hii inaweza kuwekwa wazi zaidi. "Nilipanga ya kwamba jeshi lako lingeangamiza miji na kuisababisha kuwa rundo la kifusi"

isioingilika

imara na yenye ulinzi mkali

wenye nguvu ndogo

"ambao ni dhaifu"

wamepondwapondwa

"kuvunjwa moyo"

Ninaifanya itimie

Lahaja "kufanya kitu kutimia" ina maana ya kusababisha kitu dhahiri kutokea. "Ninasababisha itokee" au "Ninasababisha vitu hivi kutendeka"

Wao ni mimea katika shamba, nyasi za kijani, nyasi juu ya paa au katika shamba, mbele ya upepo wa mashariki

Hii inazungumzia jinsi miji ilivyo dhaifu na kutoweza kujilinda mbele ya jeshi la Ashuru kwa kulinganisha miji na nyasi. "Miji ni dhaifu kama nyasi katika mashamba mbele ya majeshi yako. Wao ni dhaifu kama nyasi ambayo huota juu ya paa za nyumba na kuchomwa na upepo mkali wa mashariki"

upepo wa mashariki

Upepo wa mashariki ni wa moto na mkavu kutoka katika jangwa na mimea hufa unapovuma.