sw_tn/isa/37/21.md

1.1 KiB

akatuma ujumbe

Hii ina maana ya kwamba alituma mjumbe kutoa ujumbe kwa mfalme. "alimtuma mtu kutoa ujumbe"

ni neno ambalo Yahwe amenena

"ni kile Yahwe ambacho alisema"

anakucheka kwa kubeza

"anakucheka" au "kukudhihaki"

anatikisa kichwa chake

Hii ni ishara ya dharau.

Binti bikira wa Sayuni ... binti wa Yerusalemu

Hizi ni lahaja. Misemo hii miwili ina maana moja. "binti" wa mji ina maana watu ambao wanaishi katika mji huo. "Watu wa Sayuni ... watu wa Yerusalemu"

Ni nani umemkataa na kumtukana? ... Dhidi ya Mtakatifu wa Israeli

Yahwe anatumia maswali haya ya balagha kumkejeli mfalme wa Ashuru. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Umemkataa na kumtukana Yahwe, umepiga kelele na kutenda kwa kiburi dhidi ya Mtakatifu wa Israeli!"

umeinua sauti yako

Hii ina maana ya kuongea kwa sautii kana kwamba sauti ya mtu ilikuwa kitu ambacho walikiinua juu. "je! umepiga kelele"

kuinua macho yako kwa kiburi

Hii ni lahaja ambayo ina maana ya kutazama kitu kwa kiburi, kujichukulia muhimu zaidi kuliko unavyotakiwa. "kutazama kwa kiburi" au "alitenda kwa kiburi"