sw_tn/isa/37/11.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa Hezekia.

Tazama, umesikia

Hii ni lahaja. Neno "tazama" hapa linatumika kuongeza msisitizo kwa kile kinachosemwa baadaye. "Hakika umesikia"

Kwa hiyo utakombolewa?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kumdhihaki Hezekia na jeshi lake. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Kwa hiyo na wewe hautaokolewa" au "Kwa hiyo hakuna mtu atakayekuokoa pia!"

Je! miungu wa mataifa wamewaokoa ... Telasari?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kumdhihaki Hezekia na jeshi lake. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Miungu ya mataifa hawakukomboa mataifa ambayo baba zangu waliangamiza ... Telasari!"

ambayo baba zangu waliangamiza

Wanamume hawa waliangamiza miji iliyoorodheshwa kwa kuishinda kwa majeshi yao. Hapa neno "baba" ina maana ya baba yake na babu zake wengine ambao walikuwa wafalme. "ambao baba zangu waliangamiza kwa majeshi yao"

Gozani ... Harani .... Resefu ... Adini ... Telasari ... Hena ... Iva

Hizi ni sehemu ambazo Ashuru alizishinda.

Yuko wapi mfalme ... Iva?

Mfalme wa Ashuru hutumia swali hili kumkejeli Hezekia na jeshi lake. Hii inaweza kuandikwa kama kauli. "Pia tulimshinda mfalme ... Iva!"

Hamathi ... Arpadi ... Sefarvaimu

Haya ni majina ya miji.