sw_tn/isa/37/03.md

1.5 KiB

Walisema kwake

"Wanamume waliotumwa na Hezekia walisema kwa Isaya"

kama pale ambapo mtoto yupo tayari kuzaliwa, lakini mama hana nguvu ya kuzaa mtoto wake

Kulinganisha huku kunafanywa kusisitiza ya kwmba wapo katika kipindi kigumu sana. "Ni mateso kama siku ambapo mtoto yupo tayari kuzaliwa, lakini mama hana nguvu ya kuzaa mtoto wake"

Inaweza kuwa pale ambapo Yahwe Mungu wako atasikia maneno

Hezekia anadokeza sio moja kwa moja ya kwamba kama watu wataomba Yahwe anaweza kusikiliza na kutenda juu ya kile kamanda mkuu alichosema. Maana kamili ya kauli hii inaweza kufanywa wazi. "Huenda kama ukiomba kwa Yahwe Mungu wako atasikia ujumbe"

kamanda mku

Baadhi ya tafsiri za Biblia zinatafsiri kuwa hii ni ""Rabshake". Hili ni neno la Ashuru kwa yule mwenye nafasi ya juu kabisa ya viongozi wa kijeshi Ashuru.

bwana wake

Msemo huu una maana ya kwamba mfalme ni bwana wa kamanda mkuu.

na atakemea maneno ambayo Yahwe Mungu wako ameyasikia

Hapa msemo "maneno ambayo Yahwe Mungu wako amesikia" ina maana ya kile mfalme wa Ashuru amesema. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "na Yahwe Mungu wako atakemea mfalme wa Ashuru kwa kile alichosema"

inua maombi yako

Kuomba kwa Yahwe inaelezwa kwa njia hii kusisitiza ya kwamba Yahwe yupo mbinguni. Maombi yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa vitu ambavyo vinaweza kuinuliwa juu angani. "omba"

kwa aliyesalia ambaye bado yupo pale

Hii ina maana ya watu ambao wamebaki Yerusalemu. "kwa wachache wetu ambao bado tupo hapa"