sw_tn/isa/36/11.md

1.8 KiB

Eliakimu ... Hilkia ... Shebna

Haya ni majina ya wanamume.

Shebna

Hili ni jina la msimaizi wa kasri ya mfalme Yerusalemu

Yoa ...kamanda mkuu

Yoa ni jina la mwanamume. Kama mkuu ni mwenye nafasi ya juu kabisa ya viongozi wa kijeshi Ashuru.

Tafadhali zungumza kwa mtumishi wako

Eliakimu, Shebna, na Yoa wanajitambulisha kama watumishi wa makamanda wakuu. Hii njia ya upole ya kuzungumza na mtu mwenye mamlaka ya makubwa.

lugha ya Kiashuri, Kiyahudi

"Ashuru" ni jina la kundi la watu. "Kiashuri" ni jina la lugha yao

masikioni mwa watu ambao wapo katika ukuta

Lahaja "kuzungumza katika masikio ya mtu" ina maana ya kuzungumza pale ambapo watasikia. "ambapo watu walio juu ya ukuta waweze kutusikia"

ambao wapo katika ukuta

Hii ina maana wanasimama katika ukuta. Juu ya ukuta palikuwa papana na sehemu ambayo watu wanaweza kukaa au kusimama. Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "ambao wanasimama juu ya ukuta"

Je! bwana wangu amenituma kwa bwana wako na kwako kuzungumza maneno haya?

Kamanda mkuu anatumia swali hili kusisitiza ya kuwa ujumbe huu ni kwa ajili ya watu wote wa Yuda. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Hakika, bwana wangu amenituma kuzungumza ujumbe huu kwako na wote wanaoweza kuusikia".

Je! hajanituma kwa wanamume ambao wanakaa juu ya ukuta, ambao ... wewe?

Kamanda mkuu anatumia swali hili kusisitiza tusi lake. "Bwana wangu amenituma kwa kila mmoja anayesikia hili, ambaye atapaswa ... wewe".

watapaswa kula kinyesi chao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe pamoja na wewe

Hii ni kauli ya kuchukiza sana. Anadokeza ya kwamba watahitaji kula vitu hivi kwa sababu hawatakuwa na kitu kingine kula kwa sababu mji wao utashambuliwa. "hivi punde watahitaji kula kinyesi chao wenyewe na kunywa mkojo wao wenyewe, kama utakavyofanya, kwa sababu hautakuwa na kitu chochote cha kula"