sw_tn/isa/36/09.md

1.0 KiB

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa Hezekia kwa kuzungumnza ujumbe kwa wanamume wa Hezekia.

Unawezaje kumpinga hata nahodha mmoja ... watumishi?

Kamanda mkuu anaendelea kumdhihaki Hezekia na jeshi lake. Anaposema "unawezaje" kumaanisha Hezekia, kihalisia anamaanisha jeshi la Hezekia. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Jeshi lako hata haliwezi kushinda nahodha mmoja ...watumishi".

Basi sasa, sijasafiri hapa bila Yahwe kupigana dhidi ya nchi hii na kuiangamiza?

Kamanda mkuu anatumia swali lingine kumdhihaki Hezekia na watu wa Yuda. swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Nilikuja hapa pamoja na amri ya Yahwe kuangamiza Yerusalemu"

bila Yahwe

Hapa "Yahwe" ina maana ya amri za Yahwe. "bila amri ya Yahwe"

dhidi ya nchi hii na kuiangamiza ... Shambulia nchi hii na uiangamize

Hii ina maana kupigana dhidi ya watu na kusababisha uharibifu katika eneo ambalo wanaishi. Nchi inamaanishwa hapa ni Yerusalemu. "dhidi ya watu hawa na kuangamiza nchi yao ... Shambulia watu hawa na angamiza nchi yao"