sw_tn/isa/36/06.md

1.8 KiB

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza ujumbe wa mfalme wa Ashuru kwa Hezekia. Kamanda mkuu anazungumza ujumbe kwa wanamume wa Hezekia.

Tazama

Senakeribu anatumia lahaja kumvuta Hezekia kwa kile anachotaka kusema hivi punde.

unamtegemea Misri

Hapa "Misri" ina maana ya jeshi la Misri. "kuamini katika jesgi la Misri"

hilo tete lililochanikachanika ambalo unatumia kama gongo la kutembelea, lakini kama mtu akaliegemea, litaganda mkononi mwake na kuuchuma

Hii inazungumzia Misri, haswa jeshi lake na Farao wake, kana kwamba lilikuwa tete lililochanikachanika kusisitiza ya kwamba kuwategemea hakuwezi kuwasaidia lakini kutawadhuru tu. "hiyo ni kama kutembea kwa tete lililochanikachanika kwa ajili ya gongo. Kama mtu ataliegemea, litanga'ang'ani kwenye mkono wake na kuuchoma"

tete lililochanikachanika

tete ni shina refu la mmea kama nyasi ndefu. Kama limechanikachanika au kuharibika haliwezi kubeba uzito wowote.

gongo la kutembelea

Hiki ni kijiti ambacho mtu anaweza kutumia kama mhimili anapotembea, kimetengenezwa kwa mti wa aina yoyote ambao hukutwa njiani.

je! yeye siye yule ambaye sehemu zake za juu na madhabahu zimeondolewa na Hezekia ... Yerusalemu"?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kudhihaki watu na kuonyesha ya kwamba Yahwe alikuwa amekasirika juu ya Hezekia alichofanya na asingewalinda. Swali hili la balagha linaweza kutafsiriwa kama kauli. "yeye ndiye ambaye sehemu zake za juu na madhabahu yameondolewa na Hezekia ... Yerusalemu" au "yeye ndiye ambaye sehemu zake za juu na madhabahu ... Yerusalemu".

akamwambia Yuda na Yerusalemu, "Unatakiwa kuabudu mbele ya dhabahu hili katika Yerusalemu"?

Hii inaweza kuandikwa kama nukuu isiyo moja kwa moja. "Yuda" na "Yerusalemu" ina maana ya watu ambao wanaishi humo. "amewaambia watu wa Yuda na Yerusalemu ya kwamba wanapaswa kuabudu katika dhabahu hili tu Yerusalemu"