sw_tn/isa/36/04.md

866 B

akasema kwao

"akasema kwa Eliakimu, Shebna, na Yoa"

Chanzo cha matumaini yenu ni nini?

Mfalme wa Ashuru anatumia swali hili kutoa changamoto kwa Hezekia na kusema ya kwamba hana chanzo kizuri cha imani. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Hauna chanzo cha kutegemea cha imani yako"

kuna ushauri na nguvu kwa ajili ya vita

"una ushauri na nguvu ya kwenda vitani". Msemo "nguvu kwa ajili ya vita" ina maana ya kuwa na jeshi kubwa la kutosha na la nguvu ya kutosha yenye silaha. "una ushauri wa kijeshi wa kutosha, wanamume wenye nguvu, na silaha za kwenda vitani"

Basi sasa ni nani mnayemwamini? Ni nani kawapa ujasiri kuasi shidi yangu?

Mfalme wa Ashuru anatumia maswali kumdhihaki Hezekia kwa kuamini ya kuwa ana nguvu ya kuasi. Swali hili linaweza kuandikwa kama kauli. "Haijalishi unamwamini nani, hautakuwa na ujasiri wa kuasi dhidi yangu".