sw_tn/isa/34/05.md

1.4 KiB

pale upanga wangu utakapokuwa umekunywa ujazo wake mbinguni

Yahwe anajifafanua kama shujaa anayebeba upanga. Msemo "umekunywa ujazo wake" unazungumzia upanga wa Yahwe kana kwamba ulikuwa mtu ambaye amekula na kutosheka. Yahwe anatumia picha hii kusisitiza ya kwamba kutakuwa na uharibifu mwingi mbinguni na kutaja ukamilifu wake. "nitakapomaliiza kuangamiza vitu mbinguni"

tazama

Neno hili linatumika hapa kuwavuta wasikilizaji na kuwafanya wawaze mambo yanayosemwa. "sikiliza" au "na kisha"

sasa itashuka chini mpaka Edomu, juu ya watu naowaweka kando kwa ajili ya uharibifu

Neno "itashuka" ina maana ya upanga wa Yahwe. Hii inaendeleza sitiari kuhusu Yahwe kuangamiza vitu kwa upanga. "Nitakuja kuadhibu watu wa Edomu, watu ambao nimewaweka kando kwa ajili yangu kuangamiza"

juu ya Edomu

Edomu ina maana ya watu ambao wanaishi kule. "juu ya watu wa Edomu"

upanga wa Yahwe unadondoka kwa damu na kufunikwa na mafuta... wa kondoo dume

Hii inazungumzia Yahwe kuwaua watu kana kwamba alikuwa kuhani akitoa wanyama sadaka. Anafanya hivi kwa kufafanua upanga wa kuhani. "Yahwe anawatoa sadaka kama vile kuhani anavyotoa sadaka za wanyama, ambaye upanga wake unadondoka na damu na mafuta ya kondoo, mbuzi na kondoo dume"

Kwa maana Yahwe ana sadaka Bozra na machinjio makubwa katika nchi ya Edomu

Maneno "sadaka" na "machinjio" yanaweza kuelezwa hapa kama vitenzi. "

Bozra

Huu ni mji muhimu katika Edomu