sw_tn/isa/33/20.md

1.3 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kuzungumza na watu wa Yuda.

mji wa sikukuu zetu

Hii ina maana ya kwamba wana sikuku zao na sherehe katika mji. "mji ambapo tuna sikuku zetu" au "mji ambao tunasherehekea karamu zetu"

macho yako yataona

Watu wanajulikana kwa "macho" yao kusisitiza kile wanachoona. "utaona"

hema ambalo halitaondolewa

Hii inazungumzia Sayuni kuwa salama na kuimarishwa kana kwamba ilikuwa hema lililo salama. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda na kuandikwa kama sentensi mpya. "itakuwa salama, kama hema ambalo hakuna mtu atakayeliondoa kamwe"

ambalo viging vyake havitawah kuvutwa wala kamba zake kukatwa

Hii ni sehemu ya sitiari ambayo inalinganisha Sayuni kwa hema salama. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambalo vigingi hakuna mtu atawahi kuvivuta juu na ambalo kamba zake hakuna awezaye kuvikata"

Yahwe katika utukufu atakuwa pamoja nasi, katika sehemu ya mito mipana na vijito

Hapa "nasi" ina maana ya Isaya na inajumuisha watu wa Yuda. Hii inazungumzia usalama wa kuishi na Yahwe kana kwamba ilikuwa sehemu ambayo ina mito ikizunguka ili kwamba maadui wasiweze kuishambulia. "Yahwe ambaye ni mtukufu atakuwa pamoja nasi, na tutakuwa salama kana kwamba tupo katika sehemu inayozungukwa kwa mito mipana"

utausafiria

"utasafiri juu ya mto"