sw_tn/isa/33/10.md

1.3 KiB

inuka

"simama". Hapa neno hili lina maana ya kuanza kufanya jambo. Katika hali hii Yahwe sasa anajinua mwenyewe.

sasa nitainuliwa; sasa nitapandishwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. Misemo hii miwili ina maana moja na inasisitiza Yahwe kuinuliwa. "sasa nitajiinua na kuonyesha ya kwamba ninastahili kwa ajili ya kila mtu kuniheshimu"

Unachukua mimba ya makapi, na unazaa mashina ya mabua

Hii inazungumzia Ashuru kufanya mipango kana kwamba walikuwa wakitunga mimba na kuzaa mipango yao kama mama anavyozaa mtoto. Hii inazungumzia mipango yao kutokuwa na thamani kwa kulinganisha na majani makavu. "Unafanya mipango ambayo haina thamani kama makapi na majani makavu"

mashina ya mabua

"majani makavu"

pumzi yako ni moto ambayo itakuangamiza

Hapa mipango ya Ashuru ina maana ya "pumzi" yao. Hii inazungumzia mipango yao kusababisha wao kufa kana kwamba mipango yao ingechoma miili yao kihalisia. "mipango yako itasababisha ufe"

Watu watachomwa mpaka kuwa chokaa, kama miiba ya vichaka inavyokatwa chini na kuchomwa

Hii inalinganisha jinsi maiti za watu itakavyochomwa kwa njia ambayo vichaka vya miiba inachomwa. Pia, hi inaweza kuandikwa katika hali ya kutenda. "Moto utachoma miili ya watu kuwa chokaa kwa nja moja ambayo mkulima hukata chini vichaka vya miiba na kuvichoma"

chokaa

mjivu kutoka kwa mifupa iliyoungua