sw_tn/isa/28/18.md

1.2 KiB

Taarifa ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu.

Agano lako na kifo litayeyushwa, na makubaliano yako na kuzimu hayatasimama

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Nitafuta agano ambalo umefanya na kifo, na nitafuta makubaliano uliyofanya na kuzimu"

agano lako na kifo ... makubaliano na kuzimu

Maana zaweza kuwa 1) viongozi wa Yerusalemu wametumia mazingaombwe au uchawi kujaribu kufanya makubaliano na miungu ya sehemu za wafu ili kwamba miungu hawa wawalinde kutokufa au 2) hii ni sitiari ambayo inazungumzia viongozi kufanya makubaliano na viongozi wa Misri. Viongozi wa Yerusalemu walikuwa wanajiamini sana hadi Wamisri wangewalinda na kuonekana kana kwamba walifanya makubaliano na miungu wa sehemu ya wafu.

hayatasimama

"hayatadumu"

Pale ambapo mafuriko makali yatakapopita

Maana zaweza kuwa 1) "mafuriko" ni maneno yenye maana sawa na yanawakilisha kitu chochote kwa ujumla ambacho kitasababisha uharibifu au 2) "mafuriko" ni sitiari inayomaanisha jeshi la adui ambalo Yahwe atatuma kuangamiza watu wa Yerusalemu.

utazidiwa nayo

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "itakuzidia" au "itakuangamiza"

asubuhi kwa asubuhi

Hii ni lahaja. "kila siku"

kwa mchana na usiku

Hii ina maana "katika siku nzima"