sw_tn/isa/28/14.md

1.8 KiB

Kwa hiyo sikiliza neno la Yahwe

Isaya sasa anazungumza kwa viongozi wa Yerusalemu. Hapa "neno" linawakilisha ujumbe. "Kwa hiyo sikiliza kwa ujumbe wa Yahwe"

Tumefanya agano na kifo, na kwa kuzimu tumefikia makubaliano

Kauli hizi mbili zina maana moja. Maana zinaweza kuwa 1) viongozi wa Yerusalemu wametumia mazingaombwe au uchawi kujaribu kufanya makubaliano na miungu ya sehemu za wafu ili kwamba miungu hawa wawalinde kutokufa au 2) hii ni sitiari ambayo inazungumzia viongozi kufanya makubaliano na viongozi wa Misri. Viongozi wa Yerusalemu walikuwa wanajiamini sana hadi Wamisri wangewalinda na kuonekana kana kwamba walifanya makubaliano na miungu wa sehemu ya wafu.

Kwa hiyo mjeledi mkubwa kabisa utakapopita katikati, hautatufikia sisi

Hii inazungumzia hukumu ya Yahwe na adhabu kana kwamba ilikuwa mjeledi ambao ungewapiga watu. Na mjeledi unazungumziwa kana kwamba ulikuwa mafuriko ambayo yangepita katikati ya Yerusalemu. "Kama matokeo, ambapo wengine wote wanateseka na kufa, hakuna kitu kitatudhuru"

Kwa kuwa tumetengeneza uongo kimbilio letu, na kujiweka hifadhi katika uongo

Misemo hii miwili ina maana moja. "Uongo" unazungumziwa kana kwamba ilikuwa sehemu ambayo mtu angeweza kwenda kujificha. Viongozi wa Yerusalemu wasingesema wanatumaini katika uongo. Waliamin walikuwa salama kabisa. Lakini Isaya anajua hawako salama, kwa sababu wanaamini katika uongo. "Kwa maana uongo umekuwa kama sehemu ambayo tunaweza kujificha kutoka hatarini"

uongo kimbilio letu ... kujiweka hifadhi katika uongo

Maana zaweza kuwa 1) viongozi wanaamini katika uongo ambao wamesema ili kujilinda wenyewe au 2) viongozi huamini ya kwamba agano walilofanya na miungu ya uongo ya sehemu ya wafu itawaweka salama au 3) viongozi huamini ya kwamba makubaliano ambayo wameyafanya na Wamisri itawaweka salama.