sw_tn/isa/28/09.md

761 B

Ni kwa nani atamfundisha maarifa, na kwa nani ataelezea ujumbe?

Manabii na makuhani walevi wanatumia swali kumkosoa Isaya, ambaye anajaribu kuwasahisha. "Manabii walevi na makuhani wanasema, 'Isaya hatakiwi kujaribu kutufundisha kuhusu ujumbe wa Yahwe!'"

Kwa wale ambao wameachishwa maziwa au kwa wale ambao wameondolewa tu kutoka kwenye titi?

Manabii na makuhani walevi wanatumia swali kumkosoa Isaya, kwa sababu wanahisi ya kwamba anawafanya kama watoto. "Hatakiwi kutufanya kama watoto!"

Kwa maana ni amri baada ya amri, amri juu ya amri; utawala juu ya utawala, utawala juu ya utawala; hapa kidogo, pale kidogo

Manabii na makuhani walevi wanamkosoa Isaya kwa sababu wanahisi Isaya anarudia amri za kawaida kana kwamba alikuwa akiongea kwa mtoto.