sw_tn/isa/26/18.md

893 B

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kulinganisha mateso ya watu wa Yuda na mwanamke anayezaa.

lakini ni kana kwamba tumezaa tu upepo

"lakini ni kana kwamba tumezaa tu hewa" au "ni kana kwamba tumezaa utupu".Hii ni tashbihi ambayo inasisitiza ya kwamba mateso ya watu hayajaleta kitu chochote. "lakini hakuna kitu kizuri kilichotokana kwake"

Hatujaleta wokovu katika dunia, na wakazi wa ulimwengu hawajaanguka

Hapa "dunia" inawakilisha watu ambao wanaishi juu ya dunia. Maana haiko wazi, lakini inaonekana kumaanisha ya kwamba watu wa Israeli hawakuweza kujiokoa wenyewe au watu wengine kwa kuwashinda adui zao vitani.

Hatujaleta wokovu katika dunia

Hii inaweza kuandikwa upya ili kwamba nomino dhahania "wokovu" ielezwe kama kitenzi "kuokoa". "Hatujaokoa wakazi wa dunia"

na wakazi wa ulimwengu hawajaanguka

"wala hatujasababisha watu waovu wa ulimwengu kuanguka katika vita"