sw_tn/isa/18/06.md

1.3 KiB

Wataachwa pamoja

Inaonekana Mungu anabadilisha kutoka kuelezea fumbo na kuzungumzia moja kwa moja juu ya taifa. Hii inaweza kuwekwa wazi. "Wale ambao wanauawa wataachwa pamoja" au "Kama matawi yanayokatwa na kutupwa, miili ya wale ambao wameuawa wataachwa juu ya nchi"

Ndege watakuwa juu yao wakati wa kiangazi

"Ndege zitawala wakati wa kiangazi". Maneno "ndege" yana maana ya ndege ambao hula nyama ya miili iliyokufa.

wanyama wote wa duniani

"aina zote za wanyama pori"

watakuwa juu yao wakati wa baridi

"watawala katika kipindi cha baridi"

watu warefu na laini ... watu wanaogopwa mbali na karibu .... taifa lenye nguvu na kukanyaga chini, ambayo nchi yake imegawanywa na mito

Misemo hii yote inaelezea watu wa taifa kubwa.

watu warefu na laini

"watu ambao ni warefu na wenye ngozi laini"

watu wanaogopwa mbali na karibu

Maneno "mbali" na "karibu" yanatumika pamoja kumaanisha "kila mahali". "watu ambao wanaogopwa kila mahali" au "watu ambao kila mtu duniani anawaogopa".

taifa lenye nguvu na kukanyaga chini

Kukanyaga chini inawakilisha kushinda mataifa mengine. "taifa ambalo lina nguvu na hushinda mataifa mengine"

mpaka mahali penye jina la Yahwe wa majeshi, kwa mlima Sayuni

Neno "jina" lina maana ya Yahwe. "mpaka Mlima Sayuni, ambapo Yahwe wa majeshi hukaa"