sw_tn/isa/17/08.md

953 B

Hawataangalia katika madhabahu

Kutazama madhabahu kunawakilisha kuabudu sanama kwa tumaini ya kwamba sanamu zitawasaidia. "hawataabudu sanamu katika madhabahu yao" au "Watu wa Israeli hawatakwenda katika madhabahu yao na kuuliza sanamu zao kuwasaidia"

kazi ya mikono yao

Kuzungumzia mikono hapa inasisitiza ya kwamba watu walitengeneza madhabahu au sanamu. "ya kwamba walitengeneza kwa mikono yao" au "ambayo walitengeneza wao wenyewe"

kile vidole vyao kimetengeneza ... nguzo za Ashera au sanamu za jua

Msemo wa pili unatambua vitu ambavyo watu walitengeneza. Kuzungumzia vidole hapa inasisitiza ya kuwa watu walizitengeneza, kwa hiyo vitu hivi sio miungu ya kweli. "nguzo za Ashera au sanamu za jua, ambayo walitengeneza wao wenyewe"

walitelekezwa kwa sababu ya watu wa Israeli

Inaweza kuwekwa wazi ni nani aliacha nchi hii. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ya kwamba Wahivi na Waamori waliacha baada ya watu wa Israeli kuja"