sw_tn/isa/16/01.md

926 B

Taarifa ya Jumla

Hii inaendeleza unabii kuhusu watu wa Moabu. Mungu anaelezea matukio yatakayotokea katika siku za usoni kana kwamba yanatokea wakati wa sasa. Mstari wa kwanza huenda ndicho Mungu anasema watawala wa Moabu watasema kwao wenyewe.

Tuma kondoo dume kwa mtawala wa nchi

Wamoabu watatuma kondoo dume kwa mfalme wa Yuda ili kwamba aweze kuwalinda kutoka kwa jeshi la adui.

Sela

Hili ni jina la mji.

binti Sayuni

"binti" wa mji ina maana ya watu wa mji. "Watu wa Sayuni" au "Watu wanaoishi Sayuni"

Kama ndege wanaozurura, kama kiota kilivyosambaa, kwa hiyo wanawake wa Moabu watakuwa katika vivuko vya Mto Arnoni

Watu wote wa Moabu, ambayo inajumlisha wanawake, wanalazimishwa kutoroka kutoka kwenye nyumba zao. "Kama ndege wasio na nyumba, wanawake wa Moabu watatoroka kupitia mto hadi nchi nyingine"

Kama ndege wanaozurura, kama kiota kilivyosambaa

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja.