sw_tn/isa/14/12.md

1.0 KiB

Kauli Kiunganishi

Hii ni sehemu ya wimbo wa dhihaki ambao Waisraeli wataimba kwa mfalme wa Babeli.

Jinsi ulivyonguka kutoka mbinguni, nyota ya alfajiri, mwana wa asubuhi

Nyota ya alfajiri ni nyota inayong'aa ambayo inainuka kabla tu ya asubuhi. Watu wa Israeli watamchukulia mfalme wa Babeli kwa msemo wa hii nyota ili kuonyesha ya kwamba aliwahi kuwa mkuu, lakini sasa hayupo. "Ulikuwa kama nyota inayong'aa ya asubuhi, lakini umeanguka kutoka angani"

Jinsi ulivyokatwa chini ardhini

Watu wa Israeli watazungumzia mfalme wa Babeli kana kwamba alikuwa mti ambao ulikuwa ulikatwa chini. "Umeshindwa kama mti ambao mtu ameukata chini ardhini"

Nitakaa juu ya mlima wa kusanyiko

Hii inagusia kisasili ya kwamba watu wengi katika Mshariki ya Karibu ya Zamani, miungu wa Wakaanani walikutana baraza juu ya mlima katiika sehemu ya kaskazini ya Ashuru. Kukaa juu ya mlima inawakilisha kutawala kwa miungu. "Nitatawala juu ya mlima ambao miungu hukusanyka"

katika mipaka ya mbali ya kaskazini

"katika sehemu za kusni zaidi"