sw_tn/isa/13/15.md

1.1 KiB

Yeyote atakayepatikana atauawa ... kila mmoja ambaye anakamatwa atakufa kwa upanga

Misemo hii miwili ina maana moja. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui ataua kwa upanga kila mtu anayempata"

Watoto wao wachanga pia watakatwa vipande

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui atawakata pia watoto wao wachanga katika vipande" au "Adui atawapiga watoto wao wachanga mpaka wafe"

mbele ya macho yao

"Mbele ya macho yao" ina maana ya "katika uwepo wao" au "huku wakitazama". Inaweza kuwekwa wazi ya kwamba wazazi hawakuw\vza kuwasaidia watoto wao wachanga. "huku wazazi wao wakitazama bila msaada"

Nyumba zao zitaporwa

Hii ina maana ya kwamba kila kitu chenye thamani kitaibiwa kutoka katika nyumba zao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Adui atapora nyumba za watu" au "Adui ataiba kila kitu chenye thamani kutoka kwa nyumba za watu"

wake zao kubakwa

Hii ina maana ya kwamba maadui watashambulia wanawake na kuwalazimsha kufanya ngono pamoja nao. Maneno "watabakwa" yanaeleweka. Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "wake zao watabakwa" au "maadui wao watawabaka wake zao"