sw_tn/isa/13/13.md

513 B

Maelezo ya Jumla

Yahwe anaendelea kuzungumza.

Kama swala anayewindwa au kama kondoo asiyekuwa na mchungaji

"Kama swala ambaye hukimbia haraka pale watu wanapomwinda, na kama kondoo ambaye hana mchungaji anavyokimbia kutoka kwa wanyama pori"

swala

mnyama ambaye anafanana na mbawala. Watu huwawinda, na wanyama pori mara nyingine huwashambulia na kuwaua.

kama kondoo asiyekuwa na mchungaji

Kondoo ambao hawana mchungaji hawana mtu wa kuwalinda kutoka kwa wanyama pori ambao huwashambulia na kuwaua.