sw_tn/isa/11/03.md

2.1 KiB

Kauli Unganishi

Isaya anaendelea kumfafanua mfalme.

hatahukumu kwa kile ambacho macho yake yanaona

Msemo "kile ambacho macho yake yanaona" ina maana ya kuona vitu ambavyo sio muhimu kwa kuhukumu mtu kwa sahihi. "hatahukumu mtu kwa kumtazama tu vile ambavyo mtu anavyoonekana"

wala kuamua kwa kile masikio yake yanasikia

"na hataamua kwa kile ambacho masikio yake husikia". Msemo "kile ambacho masikio yake husikia" yana maana ya kusikia kile ambacho watu wanasema juu ya mtu. "na hatahukumu mtu kwa kusikia kile ambacho wengine wanasema juu yake"

maskini ... wanyenyekevu ... waovu

Misemo hii ina maana ya watu ambao wana sifa hizi. "watu maskini ... watu wanyenyekevu ... watu waovu"

Ataipiga dunia kwa fimbo ya kinywa chake ... kwa pumzi ya midomo yake atawachinja waovu

Misemo hii miwili kimsingi ina maana moja.

Ataipiga nchi kwa fimbo ya kinywa chake

Neno "nchi" hapa linawakilisha watu wa dunia. Kuwapiga kwa fimbo ya kinywa chake inawakilisha kuwahukumu, na hukumu hiyo italeta adhabu. "Atahukumu watu wa dunia, na wataadhibiwa"

kwa pumzi ya midomo yake atawachinja waovu

"pumzi ya midomo yake" inawakilisha yeye kuwahukumu. "atahukumu watu waovu, nao watauwawa"

mkanda wa kiuno chake ... mkanda unaozunguka kiunoni kwake

Maana zaweza kuwa 1) mkanda unatumika kuimarisha nguo za mtu ili aweze kufanya kazi, au 2) mkanda ni nguo ya ndani, au 3) mkanda ni mshipii ambao mfalme huvaa kuonyesha mamlaka yake.

Haki itakuwa mkanda wa kiuno chake

Kuvaa haki kama mkanda inawakilisha kuwa mwenye haki. Maana zaweza kuwa 1) haki ya mfalme itamuwezesha kutawala. "Haki yake itakuwa kama mkanda unaozunguka kiuno chake" au 2) haki ya mfalme itaonyesha mamlaka yake ya kutawala. "Atatawala kwa haki"

uaminifu mkanda unaozunguka nyonga yake

Maneno "utakuwa" inaeleweka katika msemo huu. "uaminifu utakuwa mkanda unaozunguka nyonga yake"

uaminifu mkanda unaozunguka nyonga yake

Kuvaa uaminifu kama mkanda inawakilisha kuwa mwaminifu. Maana zaweza kuwa 1) uaminifu wa mfalme utamwezesha kutawala, au 2) uaminifu wa mfalme utaonyesha mamlaka yake ya kutawala. "uaminifu wake utakuwa kama mkanda unaozunguka nyonga yake" au "atatawala kwa uaminifu"