sw_tn/isa/10/26.md

1.5 KiB

Yahwe wa majeshi

Yahwe wa majeshi wa Israeli

atainua mjeledi dhidi yao

"atapiga Ashuru kwa mjeledi". Mungu hatatumia mjeledi kihalisia. Hii ina maana ya nguvu ya Mungu kuadhibu Ashuru kwa ukalii. "nitaadhibu Ashuru kwa ukali kana kwamba kwa mjeledi"

kama pale alipowashinda Midiani katika mwamba wa Orebu

Hii ina maana ya pale Mungu alipomsaidia mtu aliyeitwa Gideoni kuwashinda jeshi la Midani.

Atainua fimbo yake juu ya bahari na kuinua kama alivyofanya kwa Misri

Hii ina maana ya fimbo pale Mungu aliposababisha maji ya Bahari ya Shamu kugawanyika ili watu wa Israeli waweze kutoroka kutoka kwa jeshi la Misri na ili kwamba jeshi la Misri lizame ndani yake. "Atakusaidia kutoroka kutok katika jeshi la Ashuru kama alivyowasaidia mababu zako kutoroka jeshi la Misri"

mzigo wake unainuliwa kutoka kwenye bega lako na nira yake kutoka shingoni mwako

"Yahwe atabeba mzigo ambao Ashuru ameweka katika bega lako, na atatoa nira ambayo wameweka juu ya shingo yako". Misemo hii miwili ina maana moja. Maneno "mzigo" na "nira" ina maana ya utumwa. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Yahwe ataondoa Ashuru ambaye huwakandamiza na atawazuia kuwafanya kuwa watumwa"

nira itaangamizwa kwa sababu ya unene

Msemo huu unaashiria ya kwamba shingo ya mnyama ambayo inavaa nira itakuwa nene sana kutosha nira tena. Hii ni sitiari kwa Israeli kuwa na nguvu sana hadi Ashuru kutowatawala tena. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "shingo yako itakuwa nene sana hadi itavunja nira" au "mtakuwa na nguvu sana hadi hamtakuwa tena watumwa wa Ashuru"