sw_tn/isa/10/24.md

837 B

Ashuru

Isaya anazungumzia mfalme wa Ashuru na jeshi lake kana kwamba alikuwa mtu mmoja. "mfalme wa Ashuru na jeshi lake"

Atakupiga kwa fimbo na kuinua gongo lake dhidi yako

Neno "lake" ina maana ya "Ashuru", utambulisho wa mfalme wa Ashuru na jeshi lake. Maneno "fimbo" na "gongo" ina maana ya vipande vya mbao ambavyo watu hutumia kama rungu kupiga wanyama na watu wengine. Isaya anazungumzia njia ambayo Ashuru atatawala juu ya Waisraeli kana kwamba Ashuru alikuwa akiwapiga Waisraeli kwa rungu. "Ashuru atatawala juu yako na kukufanya mtumwa"

kama Mmisri alivyofanya

Maana kamili inaweza kuwekwa wazi. "kama Wamisri walivyotawala juu ya mababu zako na kuwafanya watumwa"

hasira yangu utapelekea uharibifu wake

Nomino dhahania "uharibifu" unaweza kutafsiri kama kitenzi. "Nitamwangamiza kwa sababu nina hasira juu yake"