sw_tn/isa/10/17.md

1.7 KiB

Nuru ya Israeli itakuwa moto

Msemo "nuru ya Israeli" ina maana ya Yahwe. Haipo wazi kama Yahwe an Isaya anazungumza. "Mimi, Yahwe, nuru ya Israeli, atakuwa kama moto"

moto

"Moto" unasisitiza nguvu ya Yahwe kuangamiza kila kitu ambacho hakimpi utukufu.

Mtakatifu wake mwale

"Mimi, Yahwe, Mtakatifu wa Israeli, atakuwa kama mwale".

utaunguza na kumeza miiba na mibigili yake

"Moto utaunguza na kumeza miiba na mibigili ya mfalme wa Ashuru" Msemaji analinganisha jeshi la mfalme wa Ashuru kwa miiba na mibigili. Hii inasisitiza ilivyo rahisi kwa Mungu kuwaangamiza. "Nitaangamiza Ashuru kama moto unaochoma miiba na mibigili"

miiba ... mibigili

Maneno "mibigili" na "miiba" yote yana maana mimea isiyo na thamani y miiba; inaweza kutafsiriwa kutumia msemo mmoja.

Yahwe atateketeza utukufu wa msitu wake na nchi yake inayozaa

Maana zaweza kuwa 1) "Yahwe ataangamiza misitu mikubwa na mshamba katika taifa la Ashuru" au 2) "Yahwe ataangamiza jeshi la Ashuru kama moto unavyochoma misitu mikubwa na mashamba"

zote nafsi na mwili

Maana zaweza kuwa 1) hii inasisitiza ya kwamba Mungu ataangamiza kabisa misitu na mshamba. "kabisa" au 2) hii ina maana Mungu atangamiza kabisa watu wa Ashuru. Msemo "nafsi na mwili" ina maana ya sehemu ya roho na sehemu ya mwili ya mtu.

itakuwa kama pale maisha ya mtu mgonjwa unavyotokomea

Hii inalinganisha aidha misitu na mashamba ya Ashuru au jeshi la Ashuru kwa mtu mgonjwa anapolala kitandani akifa. Hii inasisitiza jinsi jambo kubwa sana linaweza kuwa dhaifu na kufa. "watakuwa kama mtu mgonjwa anayekuwa dhaifu na kufa"

Masalio ya miti y msitu wake utakuwa mchache sana

"Vile vinavyosalia vya miti katika msitu wa mfalme vitakuwa vichache sana"