sw_tn/isa/10/14.md

1.2 KiB

Maelezo ya Jumla

Yahwe bado anamnukuu mfalme wa Ashuru.

Mkono wangu umekamata

Mkono ni mfano wa maneno kwa nguvu ya mfalme au jeshi lake. "Katika nguvu yangu nimekamata" au "Mkono wangu umekamata"

Mkono wangu umekamata, kama katika kiota, utajiri wa mataifa

Mfalme wa Ashuru analinganisha kuchukua hazina kutoka katika mataifa kwa mtu anayechukua mayai nje ya kiota cha ndege. Hii inasisitiza jinsi ilivyo rahisi kwake na jeshi lake kushinda falme hizi zingine. "Jeshi langu limeiba utajiri kutoka mataifa kwa urahisi kama mwanamume anayechukua mayai kutoka kwenye kiota"

na kama mtu anayekusanya mayai yaliyotelekezwa, nilikusanya dunia yote

"na vile tu kama mtu anayechukua mayai kutoka katika kiota pale ndege hayupo kuyalinda, jeshi langu limechukua hazina ya kila taifa"

Hakuna aliyepigapiga mabawa au kufungua mdomo wao au kulia

Hii inalinganisha mataifa kwa ndege ambaye hukaa kwa utulivu huku mayai yake yanachukuliwa. Hii inasisitiza ya kwamba mataifa hayakufanya kitu wakati jeshi la Ashuru lilipochukua mali zao zote. "Na kama ndege ambaye hatoi sauti au kupiga mabawa yake pale mtu anapoiba mayai yake, mataifa hayakufanya chochote tulipokuwa tukichukua hazina zao"