sw_tn/isa/09/18.md

845 B

Uovu unawaka kama moto; unameza mibigili na miiba; pia unawasha vichaka vya msitu

Matendo ya uovu ya watu yanazungumziwa kana kwamba yalikuwa moto mharibifu kabisa. Moto huu huchoma hata mibigili na miiba, mimea ambayo huota katika maeneo ambayo hawaishi tena, na "vichaka vya msituni" ambapo hakuna mtu aliyewahi kuishi, kwa sababu ulikuwa umeangamiza maeneo ambapo watu walikuwa wakiishi.

mibigili ... miiba

Maneno "mibigili" na "miiba" yote ina maana mimea ya miiba isiyo na thamani; inaweza kutafsiriwa kutumia neno moja. "vichaka vya miiba"

Katika ghadhabu ya Yahwe wa majeshi nchi inachomwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kama moto ambao unachoma nchi, hasira kali ya Bwana itaangamiza watu wa Israeli"

Hakuna mtu amwachaye ndugu yake

"Hakuna mtu afanyaye kitu chochote kusaidia mtu mwingine yeyote kutoroka"