sw_tn/isa/09/04.md

1.8 KiB

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi ambacho Mungu ataokoa watu wa Israeli. Ingawa matukio haya yatatokea katika kipindi cha usoni. Isaya anayafafanua kana kwamba yalikuwa yametokea tayari. Hii inasisitiza ya kwamba hakika itatokea.

Kwa maana nira ya mzigo wake ... umeharibika kabisa kama katika siku ya Midiani

Isaya anazungumzia Waisraeli, ambao ni watumwa wa Ashuru, kana kwamba walikuwa ng'ombe anayevaa nira. Hii itatokea katika siku za usoni, lakini anazungumza kana kwamba tayari imetokea tayari. "Kwa maana kama katika siku ya Midiani utawaweka watu wa Israeli huru katika utumwa kwa wakandamizaji wao kama mtu anavyotoa nira kutoka mabegani mwa mnyama"

Kwa maana nira ya mzigo wake .... bega lake ... mkandamizaji wake

Isaya anazungumzia watu wa Israeli kana kwamba walikuwa mtu mmoja. "Kwa maana nira ya mzigo wao ... mabegani mwao ... wakandamizaji wao"

mhimili katika bega lake

Mhimili ni sehemu ya nira ambayo huenda juu ya mabega ya ng'ombe

mhimili

Maana nyingine yaweza kuwa "gongo", kipande kirefu cha mbao ambacho mtu hutumia kupiga ng'ombe ili wafanye kazi na ishara ya nguvu ya mtu kutawala watu wengine.

kiboko cha mkandamizaji wake

Isaya anazungumzia nguvu ya mkandamizaji ambayo anayo juu ya watu wa Yuda kana kwamba kilikuwa kipande cha mbao kilichotumiwa kupiga ng'ombe ili aweze kufanya kazi.

kama katika siku ya Midiani

Neno "siku" ni lahaja ambayo inaweza kumanisha tukio ambalo linachukua zaidi ya siiku moja kufanyika. "kama pale mlipowashinda Wamidiani"

kila buti inayokanyaga katika ghasia na mavazi yaliyobiringishwa katika damu yatachomwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "utachoma buti za wanajeshi na nguo zao, ambazo zimefunikwa na damu"

yatachomwa, mafuta kwa ajili ya moto

Hii inaweza kuwekwa wazi kwa kutafsiri kama sentensi mpya. "kuchomwa. Utafanya buti na mavazi mafuta kwa ajili ya moto"