sw_tn/isa/08/19.md

2.4 KiB

Maelezo ya Jumla

Isaya anazungumza

Watasema kwako, "Shauriana na watu wanaowasiliana na mizimu na wachawi", wale ambao hulia na nung'unika dua. Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai? Kwa sheria na kwa ushuhuda!

Maana zingine zaweza kuwa 1) "Watasema kwako, 'Watashauriana na wanaowasiliana na mizimu na wachawi, wale ambao hulia na ung'unika dua. Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai? Kwa sheria na kwa ushuhuda!'" au 2) "Watakaposema kwako, 'Watashauriana na wanaowasiliana na mizimu na wachawi, wale ambao hulia na ung'unika dua. Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai? Kwa sheria na kwa ushuhuda!

Watasema kwako

Neno "watasema" lina maana ya wale ambao humtumaini Yahwe. Neno "kwako" ni wingi na lina maana ya wale ambao wanamtumaini Yahwe.

Shauriana na watu wanaowasiliana na mizimu na wachawi

"Waulize wanaowasiliana na mizimu na wachawi unachpaswa kufanywa"

wanaowasiliana na mizimu na wachawi

wale ambao hudai kuzungumza na wale ambao wameshakufa

wale ambao hulia na nung'unika dua

Maneno "hulia" na "nung'unika" yana maana ya sauti ambazo wanaowasiliana na mizimu na wachawi hufanya wanapojaribu kuzungumza na wafu. "wale ambao hunong'oneza na kunung'una maneno yao ya kichawi kujaribu kuzungumza na watu waliokufa"

hulia

kufanya sauti kama ya ndege

Lakini watu wasitafute ushauri kwa Mungu wao? Je! watafute ushauri kwa wafu kwa niaba ya walio hai?

Maswali haya yanaonyesha ya kwamba watu wanaweza kushauriana na Mungu badala ya matendo yao ya kipumbavu ya kujaribu kuzungumza na watu waliokufa. "Lakini watu wanapaswa kumuuliza Yahwe kuwaongoza. Hawapaswi kutafuta majibu kutoka kwa wale waliokufa"

Kwa sheria na kwa ushuhuda!

Maana zaweza kuwa 1) "Kuwa makini na maelekezo ya Mungu na mafunzo" au 2) "Kisha unatakiwa kukumbuka mafundisho na ushuhuda niliokupatia"

sheria

Hili ni neno hilo hilo lililotafsiriwa "kumbukumbu halali" katika 8:16

ushuhuda

Inaweza kuwa Isaya au Yahwe. Ni vyema kuacha kiwakilishi kuwa na maana nyingi.

Iwapo hawatasema vitu hivi

"Kama hawatazungumza juu ya sheria na ushuhuda"

ni kwa sababu hawana nuru ya alfajiri

Isaya anazungumzia watu ambao hawamjui Mungu kana kwamba walikuwa watu wanaotembea katika giza bila mwanga wowote. "ni kwa sababu wao ni kama mtu aliyepotea gizani"