sw_tn/isa/07/20.md

1.5 KiB

Maelezo ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua kipindi ambacho jeshi la Ashuru litavamia Israeli.

Bwana atanyoa kwa wembe ambao ulikodiwa upande wa pili wa Mto Frati - mfalme wa Ashuru

Neno "wembe" ni sitiari kwa ajili ya mfalme wa Ashuru na jeshi lake, na Yahwe anazungumzia mfalme kana kwamba mfalme alikuwa mwanamume ambaye angefanya kazi ya Yahwe na kisha kupokea fedha kutoka kwa Yahwe. "Bwana atamuita mfalme wa Ashuru kutoka ng'ambo ya Mto Frati kufanya kazi kwa ajili yake kukunyoa"

ambao ulikodiwa

Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "ambao alinunua"

kichwa ... nywele za miguuni ... pia ... ndevu

Ilikuwa vibaya kwa mtu kunyoa sehemu ya juu ya kichwa chake; ilikuwa vibaya zaidi kwa mtu kunyoa "nywele za miguu"; ilikuwa vibaya kuliko zote kwa mtu kunyoa ndevu.

kichwa ... nywele za miguuni ... ndevu

Isaya hasemi ni kichwa cha nani, nywele, na ndevu ambazo Bwana anakwenda kunyoa, lakini Ahazi na msomaji wataelewa ya kwamba huyu ni mwanamume; mwanamume ni sitiari kwa ajili ya watu wanaoishi katika nchi ya Yuda.

kichwa

"nywele katika kichwa"

nywele za miguuni

Maana zaweza kuwa 1) hii ni njia ya upole kuzungumza juu ya nywele katika sehemu ya chini ya mwili au 2) hii inazungumzia nywele katika miguu.

pia itafyeka

"wembe utafyeka pia". Iwapo lugha yako inahitaji mtu kuwa mhusika wa "atafyeka", unaweza kusema, "Bwana pia atafyeka".

kwa sababu y wingi wa maziwa ambayo watayatoa

Nomino dhahania "wingi" unaweza kutafsiriwa kama kishazi. "kwa sababu watatoa maziwa mengi sana"