sw_tn/isa/06/01.md

1.2 KiB

alikuwa juu na kunyanyuliwa

Maneno "juu" na "kunyanyuliwa" yanasisitiza ya kwamba kiti cha enzi kilikuwa juu sana na juu ya kila kitu kukizunguka. Urefu wa kiti cha enzi unawakilisha jinsiu Bwana alivyo mkuu na mwenye nguvu.

ulijaza hekalu

"ulijaza kasri". Neno linalotumika kwa ajili ya hekalu hapa mara kwa mara linatumika kumaanisha kasri ya wafalme.

Juu yake palikuwa na maserafi

Neno "maserafi" ni wingi wa serafi. Hii ina maana Bwana alikuwa amekaa juu ya kiti cha enzi na maserafi walikuwa wamesimama au wakipaa karibu na Bwana tayari kumtumikia.

maserafi

Neno hili linaashiria ya kwamba viumbe hawa wanaweza kuwa na muonekano wa ukali au kufanana na nyoka. Kwa sababu hatujui haswa nini "maserafi" inamaanisha, unaweza kutafsiri hili kama "viumbe wa mabawa" au "vitu vyenye uhai vyenye mabawa". Au unaweza kuazima neno na kutumia katika lugha yako.

kila mmoja wao alikuwa na mabawa sita

"kila serafi alikuwa na mabawa sita" au "kila kiumbe alikuwa na mabawa sita"

na mawili kila moja likifunika uso wake, na mawili yakifunika miguu yake, na mawili alipaa

Maneno "mabawa" na "serafi" yanaeleweka. "kwa mabawa mawili kila serafi alifunika uso wake, na kwa mabawa mawili alifunika miguu yake, na kwa mabawa mawili alipaa"