sw_tn/isa/05/27.md

1.4 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anaendelea kufafanua jeshi ambalo litashambulia Yuda. Anafafanua kana kwamba tayai lilikuwepo.

huchoka ... huanguka ... husinzia ... hulala

Maneno haya manne yanaendelea kutoka kwenye kuchoka na kazi kwenda kutoweza kutembea vizuri, kwenda kutoweza kubaki macho, hadi kulala kabisa, kwa hiyo yote manne hutokea katika tafsiri.

Wala mikanda yao haijalegea

Wanajeshi waliweka nguo zao hali ya kubana ili iwe rahisi kusogea na kupigana.

mikanda ya ndara zao

"mikanda ya ndara zao"

kwato za farasi wao ni kama jiwe gumu

"kwato zao ni kama jiwe gumu". Isaya analinganisha sehemu ngumu ya mguu wa farasi kwa jiwe gumu, ambalo linaweza kusababisha cheche linapopigwa. Maana zaweza kuwa 1) Isaya analinganisha kwako zao ili kufafanua picha ya kutisha ya miguu yao kusababisha cheche wanapokimbia au 2) Isaya analinganisha kwato kwa jiwe gumu kusisitiza jinsi kwato zao ziilivyo na nguvu na zinavyomuwezesha farasi kufanya chochote bwana wake anachotaka kufanya.

na magurudumu ya vibandawazi vyao ni kama dhoruba

Isaya analinganisha matairi ya kibandawazi na dhoruba ili kuonyesha ya kwamba wataangamiza kila kitu katika njia yao. "na magurudumu ya vibandawazi yatazunguka kama dhoruba ya upepo"

magurudumu ya kibandawazi

Magurudumu haya mara kwa mara yana upapa uliochongoka ulionganishwa kwao ambao hukata mtu yeyote ambaye atapita karibu yake.