sw_tn/isa/05/25.md

1.2 KiB

hasira ya Yahwe imewashwa

Isaya anazungumzia hasira ya Yahwe kana kwamba ilikuwa moto. "Yahwe ana hasira sana"

Amenyosha nje kwa mkono wake dhidi yao na amewaadhibu

Nabii anazungumza kuhusu siku za usoni kana kwamba imekwsha tokea. Anafanya hivi kusisitiza ya kwamba unabii utatokea kwa hakika. "atawaadhibu kwa mkono wake wenye nguvu"

amenyosha nje kwa mkono wake dhidi yao

Hapa "mkono" una maana ya nguvu ya Mungu na utawala. "ameonyesha nguvu yake dhidi yao"

mizoga

"miili iliyokufa"

mizoga yao ni kama takataka katika mitaa

Miili iliyokufa inaruhusiiwa kulala chini mitaani kana kwamba ilikuwa takataka. Hii inaonyesha ya kwamba wengi watakufa lakini hakuna mtu atakayekuwepo kuwazika. Neno "takataka" linaweza kutafsiriwa kama "iliyokataliwa" au "mbolea".

Katika haya yote, hasira yake haizimiki, badala yake, mkono wake

"Ingawa vitu hivi vyote vimetokea, bado ana hasira, na mkono wake"

mkono wake bado unanyoshwa nje

Hapa "mkono" unawakilisha nguvu na utawala wa Mungu. Isaya anazungumza kana kwamba Yahwe alikuwa mtu aliyekuwa tayari kumpiga mtu mwingine kwa ngumi yake. Hii ni sitiari kwa ajili ya Yahwe kuadhibu Israeli. "bado atakuwa tayari kuwaadhibu"