sw_tn/isa/05/07.md

1.5 KiB

Taarifa ya Jumla

Isaya anafafanua fumbo la shamba la mizabibu.

Kwa ajili ya shamba la mizabibu la Yahwe wa majeshi ndiyo nyumba ya Israeli

"Kwa maana shamba la mizabibu la Yahwe wa majeshi linawakilisha nyumba ya Israeli" au "Watu wa Israelii ni kama shamba la mizabibu la Yahwe, Bwana wa majeshi ya malaika"

nyumba ya Israeli

Mataifa na makundi ya kikabila yanazungumziwa mara kwa mara katika Biblia kana kwamba yalikuwa nyumba, yaani, familia. "watu wa Israeli"

mtu wa Yuda mmea wake wa kufurahisha

"watu wa Yuda ni kama shamba la mizabibu ambalo huwapa watu starehe"

mtu wa Yuda

Hapa "mtu" inawakilisha watu wote wa Yuda. "watu wa Yuda"

alisubiri kwa ajili ya haki, lakini badala yake, kukawa na mauaji

Hii inaweza kubadilishwa ili kwamba nomino dhahania "haki" iweze kuelezwa kwa kitenzi "fanya kilicho haki". Nomino dhahania "mauaji" iuanweza kuelezwa kama "walijiua wao kwa wao". Yahwe alisubir watu kufanya kilicho haki, lakini badala yake walijiua wao kwa wao"

kwa ajili ya haki

Msemo "alisubiri" umeachwa lakini unaeleweka. Taarifa hii inayoeleweka inaweza kufanya maana kuwa wazi. "Alisubiri kwa ajili ya haki" au "Alisubiri kwa ajili yao kufanya kilicho haki"

badala yake, kelele za msaada

"badala yake, kulikuwa na kelele za msaada". Sababu ya watu kupiga kelele ya msaada inaweza kuwekwa wazi. "badala yake, wale ambao walikuwa dhaifu walipiga kelele kwa mtu kuwasaidia kwa sababu wengine walikuwa wakiwashambulia"

kelele

Msemo huu huenda una maana ya kelele nyingi.